TUBUNI UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA



Ipo siri kubwa katika Ufalme wa Mungu. Siri ya Ufalme wa Mungu anaijua Mungu mwenyewe. Hutufunulia yeye mwenyewe inavyompendeza. Hotuba ya kwanza ya mlimani Yesu alianza kuhubiri habari za Ufalme wa Mungu. Alitufundisha jinsi ya kuurithi Ufalme wa Mungu pia, aina ya watu wanaostahili na alitaja makundi mbalimbali kwa kusema.
“Heri wenye moyo safi maana hao watamwona MUNGU” Mathayo 5:8.
-        Wale wanaojishusha na kumtafuta Mungu kwa bidii, kwa unyenyekevu na uvumilivu, wana heri kwa sababu hatimaye wataurithi Ufalme wa Mbinguni.
-        Kila alipokwenda aliwaambia, “Tubuni ufalme wa Mbinguni umekaribia”. Waliotubu walipita na wapo Mbinguni.
-        Yohana naye alifundisha na kusema “Tubuni Ufalme wa Mungu umekaribia” na kumtengenezea Yesu njia. Waliotubu walipita na wapo Mbinguni. Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema, tubuni maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia. Mathayo 3:1-2


Yesu aliwaambia mitume na wafuasi wake; kila mtakapofika hubirini Ufalme wa Mungu, semeni hivi “Tubuni Ufalme wa Mbinguni umekaribia”. Nao waliotubu walipita wakaenda mbinguni.


       Tokea wakati huo Yesu alianza kuhuiri, na kusema, Tubuni kwa maana ufalme wa Mbinguni umekaribia Mathayo 4:17

Katika hotuba alizozifanya Mlimani alikuwa akizungumzia na kukazia kuhubiri Ufalme wa Mbinguni na alihubiri siri nyingi za Ufalme wa Mbinguni.
       Katika Mathayo 24:1-51. Yesu alizungumzia kuhusu siku za mwisho. Wanafunzi wake walipata hofu sana na kujiuliza kuhusu dalili za kurudi kwake. Baada ya kupaa kwake tazama wale wanafunzi waliendelea kuhubiri Ufalme wa Mungu. Watu wengi waliendelea kutubu na wakapita na wapo Mbinguni baada ya wale wanafunzi kuondoka duniani wengine waliendelea kuhubiri habari za Ufalme wa Mbinguni hadi sasa. Watu wengine walipotubu walipita na wapo Mbinguni. Mbingu bado haijajaa, Bwana Yesu alisema. “Mbinguni kwa baba yangu kuna makao mengi. Yohana 14:2.

Kuna wahubiri wengi wanadanganya watu kwamba Mbinguni kumeshajaa. Ingekuwa kweli Bwana Yesu asingetupa moyo ila angesema kuna kipindi mbingu zitajaa.

Injili iliendelea kuhubiriwa ikikazia watu watubu ili waweze kwenda Mbinguni hadi sasa na wengi wanapita na wanaendelea kupita. Hili Neno Ufalme wa Mbingu Umekaribia, ni Neno lenye siri kubwa kwa sababu kila linapohubiriwa watu wanaliona jipya kila siku. Na Yesu anaendelea kuvuna watu kwa mahubiri ya Neno hili “Tubuni Ufalme wa Mbinguni umekaribia”.
Yesu anakaribia kurudi.
       Sasa imefikia kwamba mavuno yanavunwa kwa wingi kwa sababu Ufalme wa Mbingu umekaribia kwelikweli (sana) katika Mathayo 24 na Isaya 24 Yesu alieleza mambo yatakayotokea siku za mwisho wakati atakapokaribia sana kurudi. (Haya maneno aliyoyasema kuhusu kurudi kwake na ishara zitakazoashiria kurudi kwake). Alisema alipokuwa haa duniani katika Mathayo 24 na alipokuwa Minguni alinena kwa kutumia kinywa cha Nabii Isaya katika sura 24. ndiyo mambo ambayo yalishaanza na yanaendelea kutokea na karibu sana yatafika ukingoni.

Sasa hii Neno “Tubuni Ufalme wa Mbinguni umekaribia” ni Neno ambalo linatakiwa lihubiriwe kwa nguvu ili kuvuna wateule wengi kwa ajili ya kuvutwa pale mawinguni. 
 

Comments